Majina ya walioomba kazi Mamlaka ya Chakula na Dawa yametoka Kwa ajili ya Usaili.
BONYEZA HAPA KUONA MAJINA
BONYEZA HAPA KUONA MAJINA
Maziwa ni moja ya chanzo muhimu sana ya lishe katika mwili wa binadamu na wanyama pia. Maziwa yana madini mengi, mafuta, vitamini pamoja na protini ambazo kwa ujumla wake zinafaida nyingi sana, na hivyo wagonjwa na wasiowagonjwa wanapaswa kunywa maziwa kila siku. Watu wanaogopa kunywa maziwa yawe ya mtindi au ''fresh'' pindi wanapougua na kutumia dawa. Maziwa ni muhimu sana kwa mtu mgonjwa.
Chanzo kikuu cha muingiliano wa dawa na maziwa ni madini yaliyomo katika maziwa yajulikanayo kwa jina la kitaalamu kama ''Calcium''. Katika mwili, madini haya yanafanya kazi ya kuimalisha mifupa na meno, ufanyaji kazi ya misuli na mfumo wa fahamu. Unapokunywa maziwa muda mfupi baada ya kumeza dawa, madini haya kuchangamana na dawa na kutengeneza kitu ambacho hakiwezi kupenya katika kuta za tumbo na kuingia kwenye damu kwa ajili ya utendaji kazi yake. Hali hii hupelekea kuwa na kiasi kidogo sana cha dawa katika damu hali ambayo inaweza kuleta matokeo hasi mfano, kutokupona (kwa sababu wadudu hawajafa), kuongeza uwezekano wa wadudu kuwa sugu dhidi ya dawa.
Unashauriwa; kunywa maziwa masaa matatu (3) hadi manne (4) baada au kabla ya kumeza dawa. Pia ikumbukwe kuwa si maziwa tu yanaweza kuleta muingiliano huu, bali hata bidhaa au chakula kilichoandaliwa na maziwa kama ''yoghurt'' inaweza kuleta matokeo yale yale.
Maziwa ni moja ya chanzo kikubwa cha mafuta (fats), baadhi ya dawa huihitaji sana mazingira ya uwepo wa mafuta futa katika kuta za tumbo ili ziweze kupenya kwa urahisi na kuingia damuni, uwepo wa dawa ya kutosha katika damu inapngeza ufanisi wa dawa. Mfano wa dawa kama hizo ni dawa maarufu sana kwa jina la mseto (Artemether lumefantrine) au ALU inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria. Unashauriwa kumeza dawa hizo na maziwa au kunywa maziwa muda mfupi baada ya kumeza dawa zenye jamii hiyo, dawa hizo hazidhuriwi na madini yaliyo katika maziwa.