
Kumekuwa na upuuzwaji mkubwa sana hasa kwa akina dada na badhi ya wanaume wanaotumia vipodozi hivyo kubadilisha rangi ya miili yao (kujichubua) ili wavutie/ wapendeze. Vipodozi hivi vina viambata sumu ambavyo vina madhara makubwa sana kwa watumiaji wake, na ni jambo linalotakiwa kutiliwa mkazo.
Baadhi ya madhara yatokanayo na vipodozi hivyo ni:-
- Kansa ya ngozi, figo, ini; figo kushindwa kufanya kazi
- Ugumba/utasa
- Magonjwa ya ngozi mf. fangasi, chunusi; mabaka; muwasho/mzio au kidonda kutopona haraka iwapo ngozi itapata jeraha au kufanyiwa upasuaji
- Kuumwa kichwa; kizunguzungu, uziwi; upofu na upotevu wa fahamu mara kwa mara.
- Magonjwa ya moyo; mishipa ya fahamu
- Mimba kuharibika au kusababisha madhara kwa mtoto tumboni mf. kuharibu ubongo
- Mwanamke kuota ndevu
- Madhara ya kiuchumi baada ya mtumiaji kuathirika

- Mercury
- Vinyl Chloride
- Chlorofluorocarbons
- Zirconium
- Steroids
- Chloroform Propellants
- Hydroquinone
- Methyl Chloride
- Bithionol
- Halogenated Salicylanilides
- Hexachlorophene
- Ikumbukwe kuwa, hata kama unapakaa kwenye ngozi, viambata hivi vina uwezo wa kupenya kwenye ngozi na kuingia ndani ya mwili, na hivyo kuleta madhara kama yaliyotajwa hapo awali. Jari afya yako, epuka vipodozi hivyo kwa usalama wa maisha yako.
No comments:
Post a Comment