Message from Authors

We give valuable information to optimize and promote rational use of medicine in popular language. Information is a powerful tool that can benefit or harm the public, we bring you information to benefit and promote health. If you do not understand Swahili, highlight the content and translate to any language to get the intended message. Follow us, subscribe and ask any question for help. Karibu.

Friday, 14 July 2017

JOB VACANCY AT MOZAMBIQUE-TANZANIA CENTRE FOR FOREIGN RELATIONS (CFR)

THE DIRECTOR OF THE CENTRE (RE ADVERTISED). - 1 POST
Employer: Centre for Foreign Relations (CFR)
Date Published: 2017-07-12
Application Deadline: 2017-07-26


JOB SUMMARY:
N/A
DUTIES AND RESPONSIBILITIES:
DUTIES AND RESPONSIBILITIES
 Maintain and promote the efficient, effective and good governance of the Centre;
  •  The Accounting Officer and Chief Spokesperson of the Centre;
  •  Principal Academic and Administrative Officer of the Centre;
  •  Secretary of the Governing Council;
  •  Implement decisions of the Governing Council;
  •  Enforce Laws and Regulations passed by the Governing Council;
  •  Formulate and implement policies to enhance the academic excellence of the Centre;
  •  Promote good relations with the Government and other Stakeholders;
  •  Facilitate and promote efficient academic activities related to training, research,
  • publications and consultancy; and
  •  Spearhead the continuous development and review of the mission, objectives and
  • policies of the Centre.
QUALIFICATION AND EXPERIENCE:
   QUALIFICATION, EXPERIENCE AND COMPETENCIES
  • Holder of Doctorate Degree in relevant fields with an excellent scholarship profile with respect to teaching, research and consultancy services to the public. 
  •  Holder of outstanding academic and administrative experiences of at least eleven (11) years in a reputable institution and capability in the area of technical education
    training.
  • He/ She should possess the ability to develop and lead an effective management team. 
REMUNERATION: Salary Scale DIRECTOR - CFR SALARY 

For details click here Instructions on how to apply for the post

Thursday, 13 July 2017

NJIA ZA KUPUNGUZA MADHARA YATOKANAYO NA UTUMIAJI WA DAWA

Katika jamii yetu kumekuwa na mazoea katika utumiaji wa dawa, bila kuzingatia kuwa dawa yeyote isipotumika ipasavyo yaweza kuwa sumu na kuleta madhara makubwa kwa watumiaji. Kumekuwa na tabia ya kununua dawa hizo iwe katika hospitali au maduka ya dawa bila kuuliza au kupewa taarifa zinazoweza kusaidia utumiapo dawa hizo. Katika aya zifuatazo, tumeainisha taarifa gani ni za msingi kwako kama mtumiaji ili kuepuka madhara yasiyokuwa ya lazima yanayoweza kutokea utumiapo dawa:-



Ongea na daktari wako, mfamasia au mtaalamu wa afya kuhusu;
  • Kitu chochote ambacho kinaweza kuathiri uwezo wako wa kutumia dawa, kama vile shida ya kumeza au kukumbuka kumeza dawa.
  • Kuwaambia kama wewe ni au unatarajia kuwa na mimba, au kama wewe unanyonyesha mtoto.
  • Daima uliza maswali yako kwa wataalamu wa afya kuhusu matatizo yoyote au mawazo unaweza kuwa nayo.
  • Kuwaambia kama una allegy au hupata athari fulani kuhusu dawa husika (Allergy and sensitivity reactions). 
Jua dawa zako unazotumia.
  • Jina la dawa
  • Mwonekano wake
  • Jinsi ya kuhifadhi  vizuri
  • Wakati, jinsi, na kwa muda gani unapaswa kutumia dawa zako
  • Hali gani ukipata wakati wa kutumia dawa unapaswa kuwaona wataalamu wa afya.
  • Nini cha kufanya kama umeruka dozi yako (missing a dose)
  • Nini unatakiwa kufanya na baada ya muda gani utarajie matokeo
  • Madhara na mwingiliano kati ya vyakula, vinywaji au dawa na dawa unazotumia na namna ya kuepuka
  • Kama unahitaji vipimo vyovyote au ufuatiliaji (tests and monitoring)
  • Daima omba uandikiwe maelezo kuhusu dawa.
Soma “Label” na fuata maelekezo
  • Hakikisha unaelewa maelekezo, uliza kama una maswali au wasiwasi.
  • Daima hakikisha kama umepewa dawa sahihi.
  • Weka dawa katika chombo cha cha awali cha kuhifadhia, wakati wote iwezekanavyo.
  • Kamwe usichanganye madawa mbalimbali katika chupa moja.
  • Soma “label” na fuata maelekezo kutoka kwa mfamasia au daktari. Ukiacha dawa au unataka kutumia dawa tofauti kuliko ilivyoagizwa, shauriana na mtaalamu wa afya kwanza.
Kuepuka mwingiliano (avoid interactions)
  • Uliza kama kuna mwingiliano na madawa mengine yoyote au virutubisho malazi (ikiwa ni pamoja na vitamini au virutubisho mitishamba), vinywaji, au vyakula.
  • Kabla ya kuanza dawa yoyote mpya au kuongeza virutubisho (ikiwa ni pamoja na vitamini au virutubisho mitishamba), uliza tena kama kuna uwezekano wa mwingiliano na dawa unayotaka kuanza kutumia.

Kufuatilia Athari za dawa  yako '- Na Madhara ya Bidhaa nyingine unazotumia
  • Kuuliza kama kuna kitu unaweza kufanya ili kupunguza madhara, kama vile kula kabla ya kumeza dawa ili kupunguza mvurugano wa dawa au kunywa maji mengi mf. Ciprofloxacin  au kula aina fulani ya chakula mf. Chakula chenye mafuta katika kutumia dawa ya malaria ijulikanayo kama mseto (ALU).
  • Kuwa makini na namna unajisikia, kumbuka mabadiliko yoyote. Andika mabadiliko ili uweze kukumbuka kumweleza daktari wako au mfamasia.
  • Kujua nini cha kufanya kama ukipata madhara na wakati wa kumwaarifu daktari au mfamasia wako.
  • Kujua wakati gani unapata nafuu kutokana na utumiaji wa dawa hiyo/hizo.
 Kupata taarifa kutoka kwa mtaalam wa afya ni haki yako ya msingi na usiogope kuuliza maswali, na hakikisha unalidhika na kuelewa maelekezo utakayopewa.

Wednesday, 12 July 2017

BAKTERIA ASABABISHAE UHARABIFU WA MIMBA

Mungu kamuumba binadamu katika hatua kuu nne (4), kuzaliwa, kukua, kuzeeka na kufa. Katika hatua hizi, kuna vikwazo mbali mbali ambavyo binadamu hukutana navyo, na moja ya jambo nyeti sana ni afya. Wasomi mbali mbali wanamitazamo tofauti juu ya lini maisha ya binadamu huanza; wengine husema maisha huanza baada tu pale yai la mwanamke linapokutana na mbegu ya kiume (fertilization), wengine husema maisha huanza baada ya mbimba kukua na kufikisha umri wa miezi mitatu (first trimester) na wengine husema maisha ya binadamu huanza baada ya kuzaliwa. Yote ni mitazamo tu ambayo inaongozwa na itikadi na misimamo mbali mbali.

Mimba ni kati ya jambo linalopaswa kupewa kipaumbe sana kutokana na asili yake. Moja ya changamoto kubwa ambayo mwanamke mja mzito hukutana nayo ni upungufu wa kinga mwilini; hii husababishwa na mabadiliko ya kifiziolojia (physiologic changes) ili mwili uweze kuzoea na kulea mimba. Hali hii huhitaji umakini mkubwa sana ili kujikinga na magonjwa mbali mbali, moja wapo ni malaria, virusi na bakteria.

Moja kati ya vimelea hatari sana kwa maisha ya mtoto aliyetumboni ni bakteria ajulikanae kwa jina la Listeria monocytogenes, bakteria huyu ana sifa zilizo tofauti sana na bakteria walio wengi, na mbaya zaidi amesahaulika na kudharaulika sana katika sekta za afya, haswa katika matibbu na vipimo kwa wajawazito. Baadhi ya sifa zake zinazomfanya kuwa tofauti ni:

Picha na themonitordaily.com. Bakteria Listeria monocytogenes
  1. Sio rahisi kumkuza katika maabara (culturing), na hivyo kupelekea kushindwa kumtambua na kumchanganya na vimelea vingine visivyokuwa na madhara
  2. Anauwezo mkubwa wa kuishi na kuzaliana vyema katika baridi la -18͒ C, bakteria wengine hawawezi kukua katika baridi kali kiasi hicho, na hivyo ana uwezo wa kuambukiza kutoka katika vyakula vilivyotunzwa vyema katika friji na tayari kwa kuliwa.
Maradhi yatokanayo na bakteria huyu (Listeriosis) yanakadiliwa kuwa 30% kwa watu walio katika hatari; wanawake wajawazito, watoto wachanga na wazee. Na kwamba takribani vifo kati ya 400 na 500 hutokea kila mwaka, ni bakteria wa tatu kuongoza kuleta maradhi yatokanayo na kula chakula chenye kimelea huyu, (food poisoning).Wajawazito na watoto wachanga, wazee na watu waliopungukiwa kinga ya mwili wapo katika hatari kubwa zaidi ya kuugua ugonjwa huu (listeriosis).

Bakteria huyu huleta madhara yapi katika mwili?
Baadhi ya madhara yasababishwayo kimelea hiki ni:-
  1. Huathiri mfumo wa ubongo (mengitis au meningoencephalitis)
  2. Vidonda katika safu za macho (corneal ulcer)
  3. Mfumo wa upumuaji na kusababisha mgonjwa kupata shida ya kupumua (pneumonia)
  4. Kuathhiri mfuko wa uzazi na mlango wa uzazi, hali hii husababisha mimba haswa iliyo na umri wa miezi mitatu (3) hadi ishirini na nne (24) kutoka, mtoto kupoteza maisha kabla ya kuzaliwa au kuzaa kabla ya wakati (mtoto njiti)
Dalili za listeriosis ni zipi?
Kwa mwanamke mja mzito atapata dalili zifuatazo:-
  •  Joto la mwili kupanda na dalili za homa kama uchovu, maumivu ya kichwa  





     Maambukizi wakati wa ujauzito na kwa mtoto mchanga yanaweza leta madhara mbalimbali yakiwemo;-
  1. Wajawazito wapo katika hatari ya kupata Listeriosis mara kumi zaidi ya watu wengine
  2. Wajawazito wenye asili ya Kihispania wapo katika hatari ya kupa Listeriosis mara 24 zaidi ya watu wengine
  3. Mbaya zaidi, wajawazito wanauwezo wa kumuambukiza mtoto aliepo tumboni mwake
  4. Ugonjwa huu wa Listeriosis unaweza kusababisha kutoa kwa mimba, kuzaa mtoto akiwa ameshakufa, kuzaa mtoto kabla ya kufikisha umri wake/mtoto njiti (Preterm labor)
  5. Ugonjwa huu unaweza sababisha mtoto mchanga kupoteza maisha.
  Kwa watu wengine (wasio na mimba), hupata dalili zifuatazo:-
  • Kukakamaa kwa shingo
  • Hali ya kuchanganyikiwa
  • Kifafa/ukakamavu wa misuli
  • Joto la mwili kupanga
  • Maumivu ya misuli
  • Kizunguzungu (loss of balance)    
Ikumbukwe kuwa bakteria huyu huathiri zaidi wajawazito, watoto wachanga, wazee na watu waliopungukiwa na kinga ya mwili
Bakteria huyu anapatikana wapi? 
Bakteria huyu hupatikana katika maeneo yafuatayo:-
  1. Mimea mbali mbali mfano, mboga za majani na matunda
  2. Mifugo mfano ng'ombe na kondoo, pamoja na mazao yake kama vile maziwa na nyama
  3. Ndege
  4. Udongo
Na hivyo ni vigumu sana kumuepuka bakteria huyu, na hivyo njia zifuatazo zitasaidia kujikinga nae:-
  1. Hakikisha unanawa mikono yako kwa sabuni kabla ya kula
  2. Hakikisha unaosha matunda kabla ya kula
  3. Hakikisha unaosha vyema mbogamboga kabla ya kuchemsha 

4. Mazingira ya kutunza nyama na machinjioni kuwa safi muda wote


 5. Hakikisha unakula vyakula vitokanavyo na maziwa yaliyotibiwa (pasteurized milk)

Ni basi, ni muhimu kuzingatia kuwa, kuhifadhi vyakula katika friji haikuepeshi na magonjwa yatokanayo na bakteria, na hivyo ni vyema kuzingatia kanuni za usafi na kuhakikisha kuwa tunakula vyakula salama kwa kulinda afya zetu, watoto, wajawazito na wazee.
Na ikumbukwe kuwa makala hii haiondoi sababu zingine zinazoweza kuleta matatizo tajwa, bakteria huyu ni moja tu ya chanzo cha matatizo hayo, hivyo ni muhimu kufika katika kituo cha afya kwa ajili ya uchunguzi zaidi.



AJIRA-CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI SHIRIKISHI MUHIMBILI (MUHAS) CHATANGAZA AJIRA 105

Chuo kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili, kimetangaza ajira 105, kwa watumishi mbali mbali, wakiwemo wauguzi, wataalamu wa maabara, watunza kumbukumbu na madereva kwa ajili ya hospitali yake mpya iitwayo Mloganzila (Mloganzila Academic and Medical centre)-MAMC
Hospitali ya MAMC
Kupata maelezo zaidi ya vigezo na namna ya kujiunga BONYEZA HAPA

Tuesday, 11 July 2017

MATUMIZI SAHIHI NA MADHARA YATOKANAYO NA MATUMIZI YASIYO SAHIHI YA DAWA


1.0 UTANGULIZI
Kwa watu wengi, matumizi ya dawa ni sehemu ya kawaida ya mara kwa mara ya maisha yao ya kila siku, na madawa haya hutegemewa kutibu ugonjwa na kuboresha afya. Ingawa dawa zinaweza kufanya wewe kujisikia vizuri na kukusaidia kupata afya njema, ni muhimu kujua kwamba madawa yote yana athari pamoja na faida zake.
Faida za dawa ni pamoja na kupunguza shinikizo la damu, kuponya maambukizi na kutuliza maumivu. Athari za dawa ni pamoja na vidonda vya tumbo au athari kubwa zaidi kama uharibifu wa ini na figo.

2.0 DAWA NI NINI?
Dawa hutumika kuuasaidia mwili dhidi ya magonjwa (kinga na kutibu), kuondoa dalili za magonjwa, kutibu majeraha na maumivu n.k.
Dawa yaweza kuwa ya asili (natural/herbal/traditional medicine) au ya kutengenezwa kiwandani(Conventional/synthetic medicine).

3.0 MATUMIZI SAHIHI YA DAWA NI NINI?
·         Ni kutumia dawa kulingana na utambuzi wa kitabibu (medical diagnosis/clinical needs) au ugonjwa husika.
·         Kutumia dawa kwa muda unaotakiwa kama ulivyoelekezwa na wataalamu wa dawa.
·         Kutumia kiasi sahihi cha dawa kama ulivyoelekezwa.
·         Kutumia dawa sahihi (proper medicine).
·         Kutumia dawa kwa usahihi (proper dose interval).

4.0 MATUMIZI YASIYO SAHIHI YA DAWA NI PAMOJA NA;
·         Matumizi ya dawa nyingi kwa mgonjwa (Polypharmacy)
·         Matumizi ya dawa za sindano wakati dawa za kumeza zingefaa zaidi
·         Kutumia dawa chini au zaidi ya dozi iliyoelekezwa.
·         Maamuzi ya kujitibu mwenyewe na tena kwa dawa isiyosahihi (self medication)
·         Kutumia dawa bila kufuata maelekezo ya mfamasia au daktari
·         Kutomaliza doseji ya dawa.

5.0 SABABU ZINAZOSABABISHA MATUMIZI YASIYO SAHIHI YA DAWA
·         Imani potofu juu ya dawa fulani/ mazoea
·         Mategemeo/mahitaji ya mgonjwa (demand/expectation from patient)
·         Kuwepo na taarifa isiyo sahihi
·         Ukosefu wa elimu juu ya athari za dawa
·         Mzigo mgonjwa(patient load lead to poor Rx)
·         Ukosefu wa wataalamu wa afya wa kutosha
·         Ukosefu wa mawasiliano kati ya wataalamu wa afya na wagonjwa.
·         Ukosefu wa vifaa vya uchunguzi; husababisha ugumu katika kutambua ugonjwa hivyo husababisha daktari kumwandikia mgonjwa dawa nyingi (lack of diagnostic facilities---promotes polypharmacy)

6.0 AINA ZA ATHARI KUTOKANA NA MATUMIZI YA DAWA.
Kuna aina kadhaa za athari kutokana na matumizi ya dawa
  • Uwezekano wa mwingiliano hatari kati ya dawa, chakula na vinywaji. Mchanganyiko wa vitu hivi inaweza kuongeza nafasi ya kuwa kunaweza kuwa na mwingiliano.
  • Uwezekano wa kwamba dawa inaweza isifanye kazi kama ilivyotarajiwa.
  • Uwezekano kwamba dawa inaweza kusababisha matatizo ya ziada.

7.0 FAIDA ZA MATUMIZI SAHIHI YA DAWA
·         Hupunguza uwezekanao wa kujenga usugu kwa vimelea kama malaria, virusi, fangasi na bacteria.
·         Hupunguza madhara ya dawa.
·         Kupunguza gharama za matibabu.
·         Hupunguza uwezekano wa kupata magonjwa yatokanayo na utumiaji sugu wa dawa.
·         Huboresha afya ya mtumiaji wa dawa.

8.0 HASARA ZITOKANAZO NA MATUMIZI MABAYA YA DAWA
·         Kujenga usugu wa vimelea mf. malaria, virusi, fangasi na bakteria dhidi ya dawa (drug resistance).
·         Husababisha magonjwa kama ugonjwa wa figo, Ini n.k.
·         Husababisha usugu wa ugonjwa (Chronicity).
·         Kuongeza madhara ya dawa( in case of overdose/over use or short dose interval than directed).
·         Upotevu wa pesa pamoja na mali- kuongeza gharama za matibabu
·         Kusababisha ulemavu (mtu mzima/kichanga)
·         Kupoteza maisha

9.0 MADHARA YANAYOWEZA KUJITOKEZA KUTOKANA NA MATUMIZI MABAYA YA DAWA (KUTOTUMIA DAWA KWA USAHIHI)
Watu wengi wamefanya dawa kuwa kama chakula au pipi! Jambo ambalo linasikitisha sana, kati ya vitu ambavyo si vyema sana kuzoea kutumia ni dawa maana dawa si rafiki wa mwili pale isipotumika ipasavyo, dawa ni sumu.
Kuna madhara mbalimbali mabli yanoyoweza kujitokeza dawa isipotumika ipasavyo, na baadhi ya madhara nimeyaongelea hapo awali. Madhara haya yanaweza kuwa ya yale yanayotokea baada ya muda mfupi au ya muda mrefu.
Madhara yanayotokea baada ya muda mfupi ni rahisi sana kuyatambua. Madhara yanayotokea baada ya muda mrefu si rahisi kuyatambua, madhara haya hutokea baada ya miaka kadhaa baad ya kutumia baada ya muda mrefu, na utapata madhara haya katika hatua fulani ya maisha yako na haitakuwa rahisi kutambua kama yamesababishwa na dawa maana pia madhara hayo hayategemei kitu kioja ili kutokea baali yanahitaji pia mambo kadhaa wa kadhaa ili yatokee.
Baadhi ya dawa zinazotumika isivyopaswa mara kwa mara katika jamii zetu ni pamoja na dawa za dawa za kutibu magonjwa yatokanayo na bacteria lakini pia kuna wimbi kubwa la ongezeko la matumizi mabaya ya dawa za kuongeza nguvu za kiume kwa vijana katika jamii zetu.

       I.  

MTAMBUE MFAMASIA WAKO

Watu wengi katika jamii ya Tanzania, inamtambua mfamasia kama mtu yeyote anaetoa dawa. Mtazamo huu si sahihi hata kidogo. Mfamasia ni mtaalamu wa dawa ambae hutoa huduma mbali mbali za kiafya mfano, ushauri kuhusu matumizi sahihi ya dawa, kufanya tafiti katika taasisi mbalimbali katika maswala yanayo husu afya haswa pale ambapo dawa zinahusishwa moja kwa moja, kusimamia utengenezaji wa dawa viwandani, kusimamia utoaji wa huduma za afya katika maduka ya dawa, n.k. Ili ukidhi vigezo vya kuwa mfamasia Tanzania, unapaswa kusajiliwa na Baraza la Famasi Tanzania kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Famasi ya Mwaka 2011.
Mfamasia katika maabra ya kuhakiki ubora wa dawa
Katika Hospitali, Mfamasia huhakikisha dawa anayopewa mgonjwa ni sahihi na inamaelezo sahihi kwa ugonjwa. Kutoa maelezo ya kina juu ya dawa ni wajibu wa mfamasia.
Wafamasia wakikagua dawa na kuziandaa kabla ya kutoa huduma kwa wagonjwa.
Kwa Tanzania Taaluma hii ya Famasi ilianzishwa takribani miaka 43 iliyopita kukiwa na chuo kimoja tu cha Dar-es-Salaam, Ikiwa kama Idara ya Famasi (Pharmacy Department) chini ya kitivo cha utabibu (Faculty of Medicine). Hivi sasa Tanzania kuna vyuo takribani vinne (4) vinavyotoa taaluma hii. Ili uweze kukidhi vigezo vya kusoma shahada ya famasi mwanafunzi anapaswa awe na ufaulu mzuri katika masomo ya Physics, Chemistry and Biology, ambayo ndo haswa kitovu cha taaluma hii.

Chini ya mfamasia kuna taaluma mbali mbali za dawa mfano Diploma in Pharmaceutical sciences, Certificate in Pharmaceutical Sciences. Na hivi karibuni Baraza la Famasi limeanzisha course fupi mbili ambazo zinajulikana kama ADDO (Accredited drug dispensing outlet) dispensers na Medicine dispensers, ili kukabidiliana na upungufu wa wataalamu wa dawa vijijini (kwa maelezo zaidi tembelea http://pc.go.tz/addo). Mfamasia husimamia wanataaluma wote hawa ili kutoa huduma sahihi ya dawa kwa wagonjwa.
Hivyo basi ni wajibu wako na ni muhimu kujua kuwa, kila mara utembeleapo katika duka la dawa lilipo mtaani, jilidhishe kuwa lina vibali halisi kutoka mamlaka husika na pia uulize taarifa mbali mbali kuhusu dawa unayopewa mfano, madhara ya kutalajia (side effects) pindi unapotumia dawa hiyo/hizo, vitu gani vya kuepuka kufanya pindi unatumia dawa hizo, na pia jilidhishe kuwa dawa hiyo haijaisha muda wake wa matumizi. Ni muhimu na ni hakiyako ya msingi, pale inapohitajika omba ukutane na mfamasia.
Hivyo ni muhimu kumtumia mfamasia ili kuepuka madhara yatokanayo na dawa.